KCWW RAM/10 1438
FADHILA ZA UHARAKISHA KUFUTURU II
Darasa ya Ramadhani, Jumatano tarehe 5 Ramadhani 1438, sawa na 31 Mei 2017
222 Mlango wa Fadhila za Kuharakisha Kufuturu, Sunna ya Kitu cha Kufuturia na Dua ya Kusoma Baada ya Kufuturu
1245. Imepokewa kutoka kwa Abu Ibrahim ‘Abdullah bin Abi Awfa رضي الله عنهما akisema: Tulisafiri na Mtume ﷺ akiwa amefunga. Jua lilipokuchwa, alimwambia mtu mmoja, “Fulani! Teremka kipando chako na tupatie uji!” Yule mtu akamjibu, “Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu! Si bora ungesubiri mpaka litande giza?”
Mtume ﷺ akamwambia, “Teremka kipando chako na tupatie uji!” Yule mtu akamjibu, “Lakini bado mchana, kweupe!” Mtume ﷺ akamwambia tena, “Teremka utupatie uji!” Yule mtu akateremka na kuwapatia uji. Na Mtume ﷺ akanywa kisha akasema, “Mkiona usiku umeingia upande huu basi wakati wa kufuturu umewadia kwa mwenye kufunga” huku akionesha kwa mkono wake upande wa mashariki. _Muttafaq ‘alayhi.
1246 Imepokewa kutoka kwa Salman bin ‘Amir Adh-Dhwabbiyy As-Swahaabiyy رضي الله عنه akisema: Amesema Mtume ﷺ, “Anapofungua mmoja wenu afungue kwa tende, akikosa tende basi afungue kwa maji, kwani maji ni kinywaji safi”. Ameipokea Abu Daud na Tirmidhi aliyesema Hadithun hasanun Swahih.
1247. Imepokewa kutoka kwa Anas رضي الله عنه akisema: “Ilikuwa kawaida ya Mtume ﷺ kufuturu kabla ya kuswali, kwa vijitende vilivyoiva (yaani bado kunyauka), zikikosekana basi hufuturu kwa tende kidogo (tende za kawaida zilizonyauka), zikikosekana basi hufuturu kwa vijifundo viwili vitatu hivi vya maji”. Ameipokea Abu Daud na Tirmidhi aliyesema Hadithun hasan.
UFAFANUZI
Hadithi za sehemu hii, kama hadithi zilizotangulia, zinatilia mkazo wakati wa kufuturu, kuharakisha kufuturu, na kufuturu kwa kitu gani.
Kwanza, jua likishakuchwa tu, basi wakati wa kufuturu umeshafika, hata kama bado kuna mwangaza angani. Kigezo ni kuchwa jua, si kutanda weusi au giza. Kwa maana hiyo, ukiwa na ala au chombo cha kuaminika, kinachokupa ishara ya kuwa jua limekuchwa, kama saa madhubuti, basi wakati wa kufungua kinywa umefika, maana kigezo ni kuchwa jua, si kutanda weusi au giza angani.
Pili, ukishahakikisha kuwa jua limekuchwa, basi jambo la kwanza kufanya ni kufungua kinywa. Acha mengine yote ufungue kinywa kwanza. Hiyo ndiyo Sunna ya Mtume ﷺ na amri yake.
Tatu, kama una tende, basi fungua kwa tende, kama huna basi tunda lolote tamu au kitu chochote kile kitamu. Kikikosekana basi hata glasi ya maji, kwani maji yanasafisha vitu vingi mwilini. Hiyo ni Sunna ya Mtume ﷺ.
Nne, Sunna ya Mtume ﷺ ni kufuturu kwanza, kisha kuswali magharibi, na si kinyume chake.
Mwisho, kuomba dua baada ya kufungua kinywa, kwani Mtume ﷺ amesema: “Dua ya mwenye kufunga hairudi mikono mitupu”. Muttafaq alayhi.
Miongoni mwa Dua ziliyopokewa kutoka kwa Mtume ﷺ ni:
اللهم لك صمت وعلى رزقك افطرت ذهب الظمأ، وابتلت العروق، وثبت الأجر إن شاء الله
“Ewe Mola wangu! Kwa ajili Yako nimefunga, na kwa riziki Yako nimefungua. Kiu kimeondoka na mishipa imerutubika, na ujira, kwa utashi wa Allah, umepatikana!”
YALIYOMO NA YATOKANAYO
1. Kuharakisha kufuturu ni Sunna ya kauli na vitendo vya Mtume ﷺ.
2. Sunna kufuturu mara tu baada ya kuhakikisha kuwa jua limekuchwa.
3. Kuchwa jua ndio kigezo cha kumalizika Swaumu ya Siku.
4. Kujuzu kufuturu kwa uji na mfano wake, ikikosekana tende.
5. Kufuturu kwa kokwa mbili tatu za tende ndiyo Sunna.
6. Ikikosekana tende, au tunda tamu, basi fungua kinywa kwa mafundo mawili matatu ya maji.
7. Tende ina virutubisho vingi vya kuchangamsha nguvu mwilini, hasa kwa mwenye kufunga.
8. Maji yana faida kubwa mwilini, hasa wakati wa kufuturu.
9. Kujuzu kufunga ukiwa safarini.
10. Kujuzu kutoa ushauri kwa Mtume ﷺ hakumaanishi kumpinga.
11. Riwaya nyengine zimefafanua kuwa aliyetoa ushauri huo alikuwa Sayyidina Bilal bin Rabah رضي الله عنه.
12. Mapenzi na hima ya Sayyidina Bilal رضي الله عنه kwa Mtume ﷺ na mapenzi ya Mtume ﷺ kwa Sayyidina Bilal رضي الله عنه.
13. Kujuzu kuwa na mtumishi msaidizi safarini.
14. Sunna ni kufuturu kwanza, kisha kuswali.
15. Umuhimu wa kufuata Sunna za Mtume ﷺ kwa kauli na vitendo.
INAENDELEA ...
والله أعلم وبالله التوفيق
الحقير إلى الله تعالى الدكتور السيد عبدالقادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم
Imetayarishwa na Sayyid Abdulqadir Shareef
Kutoka “Kitalu cha Waja Wema: Maneno ya Muokozi wa Umma”, kitabu ambacho ni tafsiri kamili ya رياض الصالحين من كلام سيد المرسلين للإمام النووي kilichotungwa na Imam An-Nawawi na kufasiriwa kwa Kiswahili na Sayyid Abdulqadir Shareef Aal Shaykh Abi Bakr bin Salim.
NI RUHUSA KUNUKUU, kama ilivyo, pasi na kubadilisha au kuongeza chochote, na kuweka kwenye FB yako, WhatsApp, na kwenye Makundi ya Mitandao ya Kijamii za Kiislamu, kwa lengo la kusambaza na kuelimisha Dini. Changia kusambaza Dini, ujipatie thawabu.
kcwajawema@gmail.com
FADHILA ZA UHARAKISHA KUFUTURU II
Darasa ya Ramadhani, Jumatano tarehe 5 Ramadhani 1438, sawa na 31 Mei 2017
222 Mlango wa Fadhila za Kuharakisha Kufuturu, Sunna ya Kitu cha Kufuturia na Dua ya Kusoma Baada ya Kufuturu
1245. Imepokewa kutoka kwa Abu Ibrahim ‘Abdullah bin Abi Awfa رضي الله عنهما akisema: Tulisafiri na Mtume ﷺ akiwa amefunga. Jua lilipokuchwa, alimwambia mtu mmoja, “Fulani! Teremka kipando chako na tupatie uji!” Yule mtu akamjibu, “Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu! Si bora ungesubiri mpaka litande giza?”
Mtume ﷺ akamwambia, “Teremka kipando chako na tupatie uji!” Yule mtu akamjibu, “Lakini bado mchana, kweupe!” Mtume ﷺ akamwambia tena, “Teremka utupatie uji!” Yule mtu akateremka na kuwapatia uji. Na Mtume ﷺ akanywa kisha akasema, “Mkiona usiku umeingia upande huu basi wakati wa kufuturu umewadia kwa mwenye kufunga” huku akionesha kwa mkono wake upande wa mashariki. _Muttafaq ‘alayhi.
1246 Imepokewa kutoka kwa Salman bin ‘Amir Adh-Dhwabbiyy As-Swahaabiyy رضي الله عنه akisema: Amesema Mtume ﷺ, “Anapofungua mmoja wenu afungue kwa tende, akikosa tende basi afungue kwa maji, kwani maji ni kinywaji safi”. Ameipokea Abu Daud na Tirmidhi aliyesema Hadithun hasanun Swahih.
1247. Imepokewa kutoka kwa Anas رضي الله عنه akisema: “Ilikuwa kawaida ya Mtume ﷺ kufuturu kabla ya kuswali, kwa vijitende vilivyoiva (yaani bado kunyauka), zikikosekana basi hufuturu kwa tende kidogo (tende za kawaida zilizonyauka), zikikosekana basi hufuturu kwa vijifundo viwili vitatu hivi vya maji”. Ameipokea Abu Daud na Tirmidhi aliyesema Hadithun hasan.
UFAFANUZI
Hadithi za sehemu hii, kama hadithi zilizotangulia, zinatilia mkazo wakati wa kufuturu, kuharakisha kufuturu, na kufuturu kwa kitu gani.
Kwanza, jua likishakuchwa tu, basi wakati wa kufuturu umeshafika, hata kama bado kuna mwangaza angani. Kigezo ni kuchwa jua, si kutanda weusi au giza. Kwa maana hiyo, ukiwa na ala au chombo cha kuaminika, kinachokupa ishara ya kuwa jua limekuchwa, kama saa madhubuti, basi wakati wa kufungua kinywa umefika, maana kigezo ni kuchwa jua, si kutanda weusi au giza angani.
Pili, ukishahakikisha kuwa jua limekuchwa, basi jambo la kwanza kufanya ni kufungua kinywa. Acha mengine yote ufungue kinywa kwanza. Hiyo ndiyo Sunna ya Mtume ﷺ na amri yake.
Tatu, kama una tende, basi fungua kwa tende, kama huna basi tunda lolote tamu au kitu chochote kile kitamu. Kikikosekana basi hata glasi ya maji, kwani maji yanasafisha vitu vingi mwilini. Hiyo ni Sunna ya Mtume ﷺ.
Nne, Sunna ya Mtume ﷺ ni kufuturu kwanza, kisha kuswali magharibi, na si kinyume chake.
Mwisho, kuomba dua baada ya kufungua kinywa, kwani Mtume ﷺ amesema: “Dua ya mwenye kufunga hairudi mikono mitupu”. Muttafaq alayhi.
Miongoni mwa Dua ziliyopokewa kutoka kwa Mtume ﷺ ni:
اللهم لك صمت وعلى رزقك افطرت ذهب الظمأ، وابتلت العروق، وثبت الأجر إن شاء الله
“Ewe Mola wangu! Kwa ajili Yako nimefunga, na kwa riziki Yako nimefungua. Kiu kimeondoka na mishipa imerutubika, na ujira, kwa utashi wa Allah, umepatikana!”
YALIYOMO NA YATOKANAYO
1. Kuharakisha kufuturu ni Sunna ya kauli na vitendo vya Mtume ﷺ.
2. Sunna kufuturu mara tu baada ya kuhakikisha kuwa jua limekuchwa.
3. Kuchwa jua ndio kigezo cha kumalizika Swaumu ya Siku.
4. Kujuzu kufuturu kwa uji na mfano wake, ikikosekana tende.
5. Kufuturu kwa kokwa mbili tatu za tende ndiyo Sunna.
6. Ikikosekana tende, au tunda tamu, basi fungua kinywa kwa mafundo mawili matatu ya maji.
7. Tende ina virutubisho vingi vya kuchangamsha nguvu mwilini, hasa kwa mwenye kufunga.
8. Maji yana faida kubwa mwilini, hasa wakati wa kufuturu.
9. Kujuzu kufunga ukiwa safarini.
10. Kujuzu kutoa ushauri kwa Mtume ﷺ hakumaanishi kumpinga.
11. Riwaya nyengine zimefafanua kuwa aliyetoa ushauri huo alikuwa Sayyidina Bilal bin Rabah رضي الله عنه.
12. Mapenzi na hima ya Sayyidina Bilal رضي الله عنه kwa Mtume ﷺ na mapenzi ya Mtume ﷺ kwa Sayyidina Bilal رضي الله عنه.
13. Kujuzu kuwa na mtumishi msaidizi safarini.
14. Sunna ni kufuturu kwanza, kisha kuswali.
15. Umuhimu wa kufuata Sunna za Mtume ﷺ kwa kauli na vitendo.
INAENDELEA ...
والله أعلم وبالله التوفيق
الحقير إلى الله تعالى الدكتور السيد عبدالقادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم
Imetayarishwa na Sayyid Abdulqadir Shareef
Kutoka “Kitalu cha Waja Wema: Maneno ya Muokozi wa Umma”, kitabu ambacho ni tafsiri kamili ya رياض الصالحين من كلام سيد المرسلين للإمام النووي kilichotungwa na Imam An-Nawawi na kufasiriwa kwa Kiswahili na Sayyid Abdulqadir Shareef Aal Shaykh Abi Bakr bin Salim.
NI RUHUSA KUNUKUU, kama ilivyo, pasi na kubadilisha au kuongeza chochote, na kuweka kwenye FB yako, WhatsApp, na kwenye Makundi ya Mitandao ya Kijamii za Kiislamu, kwa lengo la kusambaza na kuelimisha Dini. Changia kusambaza Dini, ujipatie thawabu.
kcwajawema@gmail.com
NiNimeulizwa pembeni na watu wawili tofauti, na nimewajibu pembeni, ila kwa faida ya watu wengi nimeona nitoe swali na jibu hadharani.
Nanukuu:
Salaam Alaykum Sayyid.
Nipe tafauti ya Sala ya Tahajud na sala ya Kiyamul lail
Nini Fadhila za Tahajjud na Qiyaam al-Lyl?
Nini Fadhila za Tahajjud na Qiyaam al-Lyl?
JIBU.
BISMILLAH.
Ibada yoyote, isiyokuwa ya Faradhi, inayofanywa usiku, baada ya Kuswali Ishaa na kabla ya kuchomoza alfajiri, ni Qiyaam al-Layl. Hivyo basi, قيام الليل maana yake kusimama usiku kwa ibada, au kuhuyisha usiku kwa ibada, kwa ajili ya Allah peke Yake.
Na kusimama usiku au kupitisha Usiku, siyo lazima usiku mzima au hata mwingi wake. Bali hata sehemu, tu, ya Usiku, hata kama ni masaa machache au saa moja hivi au hata nusu saa tu, kwa kufanya Ibada kama Kuswali Sunna, Kusoma Qur’ani, Kumtaja Mwenyezi Mungu, Kusoma ilimu ya Dini, kama Hadithi na Tafsiri na kadhalika. Na kila muda wa kufanya Ibada hizo unapoziidi kuwa mrefu ndipo na thawabu za Qiyaam al-Layl nazo zinapozidi na kuongezeka; na Hivyo Qiyaam al-Layl kina faida zaidi.
Kwa maana hiyo, yule aliyefanya Ibada usiku, kwa muda mrefu zaidi, ndiye mbora wa wanaofanya Qiyaam al-Layl. Na yule aliyefanya Ibada usiku, kwa muda mchache zaidi, hata kama muda wa nusu saa tu, basi ni mbora wa watu wote ambao hawakufanya ibada usiku.
Kwa maana hiyo, Qiyaam al-Layl ni ibada inayofanya usiku, na ambayo SI FARADHI.
Kwa mfano, Swala za Witri, kuanzia rakaa moja hadi kuendelea mpaka kufika 33, au 37 kwa kuziswali rakaa mbili mbili, na kumalizia rakaa moja. Au Tarawehe katika mwezi wa Ramadhani. Vivyo hivyo, Kusoma Qur’ani, iwe ndani ya Swala hizo za Sunna, au nje ya Swala hizo. Kumtaja Mwenyezi Mungu; yaani kusoma nyiradi mbali mbali. Kujifunza ilimu za Dini, kama Tafsiri na Hadithi za Mtume صلى الله عليه وسلم .
Huko ndiko kufufua au kuhuyisha au kusimama kwa Ibada Usiku, vile watu wengine wamelala fofofo wanakoroma.
Ama Tahajjud maana yake Swala ISIYOKUWA YA FARADHI, na ambayo inaswaliwa Usiku, BAADA ya kulala na kisha kuamka kwa Ibada hiyo au hizo. Kama Witri na Tarawehe.
Kwa maana hiyo, kila mwenye Kutahajjad (amelala kidogo baada ya kuswali Isha, kisha akaamka na kuswali swala za usiku) anaingia katika fadhila za Kusimama Usiku; lakini SI kila anayesimama usiku kufanya Ibada ni Mutahajjid.
Hivyo basi, kulala usiku –baada ya kuswali swala zako za faradhi (Mgharibi na Isha), kisha ukaamka kwa kufanya Swala za usiku, unakuwa UMETAHAJJAD na UMESIMAMA USIKU KUFANYA IBADA. Na mtindo huu ndio uliokuwa HULKA ya Mtume صلى الله عليه وسلم (ingawa inafaa tutambuwe kuwa Tahajjud kwa Mtume صلى الله عليه وسلم ILIKUWA WAJIBU KWAKE, YAANI KAMA FARADHI kama alivyoamwishwa na Allah afanye hivyo katika Surat al-Muzzammil, 1-6.)
Mtume صلى الله عليه وسلم alikuwa akifanya Ibada za Usiku, na kusimama kuswali swala ndefu, yaani kusoma Sura ndefu (Wakati mmoja alisoma Surat al-Baqara, Akaingia al-Imraan, akaingia al-Nisaa, katika Rakaa moja tu, kiasi kijana aliyjaribu kumfuata nyuma yake, alikaribia kumuacha akae kitako) na kuomba dua kwa muda mrefu, katika sijida, hata ikawa miguu yake inamvimba, na kutokwa na melengelenge, licha ya kwamba ameahidiwa na Mola wake kufutiwa dhambi zake zilizopita - na za baadae! (Bukhari)
Alipoulizwa na Bibi Aisha رضي الله عنها kwanini anafanya hivyo (kurefusha Swala, kwani angeliweza kuswali rakaa chache fupi tu), licha ya ahadi aliyopewa na Mola wake, alijibu kwa kusema: “Na kwanini nisiwe mja mwenye kushukuru!” (Muttafaq Alayhi)
Yaani “nataka niwe mja mwenye kumshukuru Mola wake. Kwa sababu, kama alivyosema Mwenyezi Mungu: Mkinishukuru basi Naapa nitawaongezeni!” صلى الله عليه وسلم nani kama yeye, amjuaye Mola wake na kumuabudu kikomo cha kumuabudu!
Yaani “nataka niwe mja mwenye kumshukuru Mola wake. Kwa sababu, kama alivyosema Mwenyezi Mungu: Mkinishukuru basi Naapa nitawaongezeni!” صلى الله عليه وسلم nani kama yeye, amjuaye Mola wake na kumuabudu kikomo cha kumuabudu!
Mmoja wapo wa maswahaba wa Mtume صلى الله عليه وسلم anayeitwa al-Hajjaj bin ‘Amr al-Answari رضي الله عنه alikuwa akisema kuwambia watu:
“Hivi mnafikiri kwamba mtu akisimama kidogo usiku akaswali ndiyo ameshakuwa MUTAHAJJID! Waapi! Tahajjud ni kuswali baada ya kulala, na kisha kulala tena na kuamka na kuswali tena. Na hivyo ndivyo alivyokuwa akifanya Mtume صلى الله عليه وسلم (al-Talkhiis, cha Ibn Hajar, juzuu ya 2, ukurasa 35) Hadithi hiyo ameipokea Tabarani.
Swala yoyoteya SUNNA inayoswaliwa usiku, au Dua yoyote inayoombwa usiku ni Quyaam al-Layl, na iwapo utalala baada ya Isha kisha ukaamka mahasusi kwa kuswali SUNNA za Usiku, -kama Witri- kabla ya kuchomoza alfajiri ni TAHAJJUD na, wakati huo huo
ni QIYAAM AL-LAYL.
ni QIYAAM AL-LAYL.
Kwa ufupi, Qiyaam al-Layl ni Ibada YOYOTE ifanywayo Usiku, sawa sawa uifanye kabla ya kulala, au ulale kisha uamke ufanye ibada hizo, kisha urudi tena au usirudi tena kulala, na kusubiri Swala ya Alfajiri.
Kuna Dua nyingi zilizopokewa kutoka kwa Mtume صلى الله عليه وسلم za kuomba usiku, iwe ndani ya swala ua nje ya swala. Nyingi ya dua hizo zimo kwenye kitabu cha al-Adhkaar cha Imam al-Nawawi رحمه الله na nyengine katika vitabu vya Hadithi, kama al-Targhiib wa al-Tahiib, cha Imam al-Mundhiri.
Na kuna Aya za Qur’ani na hadithi chungu nzima, zinazo zungumzia Fadhila za Qiyaam al-Layl na Tahajjud.
Kwa mfano. Mwenyezi Mungu Amewasifu wachamungu, katika Surat al-Dhariyaat kwa kusema: “Hakika wachamungu watakuwa katika mabustani yenye chemchemi. Wanapokea aliyowapa Mola wao. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema. Walikuwa wakilala kidogo tu usiku. Na kabla ya alfajiri wakiomba maghafira. Al-Dhariyaat: 15-18
Na amesema: “Hakika wanao ziamni Aya zetu ni hao tu ambao wankikumbushwa hizo, basi wao huanguka kusujudu, na kumsabihi Mola wao kwa kumshukuru, na hawajivuni. Mbazo zao zinaachana na matandiko kwa kumwomba Mola wao, kwa khofu na matumaini, na hutoa kutokana na tulivyo waruzuku. (al-Sajda: 15-16)
Kwa mfano. Mwenyezi Mungu Amewasifu wachamungu, katika Surat al-Dhariyaat kwa kusema: “Hakika wachamungu watakuwa katika mabustani yenye chemchemi. Wanapokea aliyowapa Mola wao. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema. Walikuwa wakilala kidogo tu usiku. Na kabla ya alfajiri wakiomba maghafira. Al-Dhariyaat: 15-18
Na amesema: “Hakika wanao ziamni Aya zetu ni hao tu ambao wankikumbushwa hizo, basi wao huanguka kusujudu, na kumsabihi Mola wao kwa kumshukuru, na hawajivuni. Mbazo zao zinaachana na matandiko kwa kumwomba Mola wao, kwa khofu na matumaini, na hutoa kutokana na tulivyo waruzuku. (al-Sajda: 15-16)
1. Imepokewa kutoka kwa Jabir رضي الله عنه akisema: Amesema Mtume صلى الله عليه وسلم Katika kila Usiku, huweko saa moja, ambayo iwapo mja Mwislamu atamuomba Allah, katika saa hiyo, jambo lolote lile la kidunia ua la Akhera, basi Atampa tu. Na saa hiyo imo katika kila usiku” Ameipokea Muslim, H.757.
2. Imepokewa kutoka kwa Abu Umama al-Bahiliyy رضي الله عنه akisema: Amesema Mtume صلى الله عليه وسلم “Jitahidini kusimama Usiku (kwa ibada) kwani huo ndio mtindo na hulka ya Waja wema waliokutangulieni, na ndiyo njia ya kujisogezeni karibu zaidi kwa Mola wenu, na ndiyo kifutio kikubwa cha dhambi, na kiokozi cha kuepuka dhambi” Imepokewa na Tirmidhi, H.3549, Ibn Abid-Dunya, Ibn Khuzayma, na al-Hkim, Juzuu 1, H.308.
3. Imepokewa kutoka kaw Abu Hurayra رضى الله عنه akisema: Amesema Mtume صلى الله عليه وسلم Funga iliyobora kabisa kuiko funga zote ni Funga ya Rmadhani, na Swala iliyobora kabisa, baad ya Swala za Faradhi, ni Swala za Usiku.” Muslim, H.1163; Abu Daud, H.2429; Tirmidhi, H. 740; na Nasai, H.207.
4. Imepokewa kutoka kwa Abdullah bin Sallam رضى الله عنه akisema: Alipokuja Madina Mtume صلى الله عليه وسلم watu walitoka makundi kwa makundi kwenda kumlaki, na mimi nilikuwa miongoni mwao. Basi nikauangalia uso wake kwa umakini mkubwa sana, na nikatongoa (kuelewa na kufahamu kwa undani kabisa) kuwa kamwe hawezi kuwa mtu mwongo!.Na kauli yake ya mwanzo niliyoisikia kutoka kwake ni: “Enyi wanaadamu! Toleanieni Salama (salimianeni), na wakirimuni watu chakula, na shikamaneni na ndugu na jamaa zenu, na Swalini Usiku – vile watu wamelala- mkifanya hivyo mtaingia Peponi kwa salama” (hakuna kuhesabiwa) Tirmidhi, H. 2885; Ibn Majah,H.3251; al-Hakim, 3\12.
5. Imepokewa kutoka kwa Asmaa’ bint Yazid رضي الله عنها akisema: Amesema Mtume صلى الله عليه وسلم “Watafufuliwa Watu katika Janwa moja, Siku ya Kiyama. Na kutanadiwa (Wataitwa) “Wawapi waliokuwa wakiinua mbavu zao kutoka kwenye matandiko yao (ya kulalia)?” Basi watatokeza, na watakuwa watu wachache tu (kulingana na umati wa watu). Basi wataingizwa Peponi pasi na kuhesabiwa, na waliosalia wataamrishwa kuelekea kwenye sehemu ya kuhesabiwa (kwa amali zao). Al-Bayhaqi, Shu’ab al-Iiman, H. 3244. Al-Targhiib wa al-Tarhiib:H.9\901
Kwa maana hiyo, swala maalum, ambayo inaswaliwa muda maalum, tena usiku, huitwa Tahajjud. Kama Witri na Tarawehe. Swala hizi mbili zinaswaliwa Usiku tu. Vile Witri inaswaliwa kila siku usiku baada ya isha, Tarawehe inaswaliwa usiku baada ya Isha katika Mwezi wa Ramadhani. Ndiyo maana Swala hizo mbili hazikimiwi, kama Iqama ya Swala za Faradhi, bali hunadiwa tu: Swalaatul-Layl, al-Swalaatu Jaami’ah, iwapo inaswaliwa jamaa.
Ama mtu akiswali peke yake, basi hakuna haja ya kunadi chochote, anasimama na kuswali Witri zake au Tarawehe peke yake, katika mwezi wa Ramadhani.
Na Tahajjud na Qiyam al-Layl LAZIMA zifuatiwe na Swala ya Alfajiri. Hakuna sababu kuswali Sunna za usiku, lakini ikiingia alfajiri unakwenda kulala.
Au unaamka kwa Thajjud kisha unakwenda kulala huamki kwa Swala ya Alfajiri. Tahajjud yako haina faida, kwako, na qiyaam al-Layl yako, vile vile, haina faida.
Au unaamka kwa Thajjud kisha unakwenda kulala huamki kwa Swala ya Alfajiri. Tahajjud yako haina faida, kwako, na qiyaam al-Layl yako, vile vile, haina faida.
NYONGEZA. Tahajjud au Qiyaam al-Layl ni Sunna ya kudumisha, kadiri ya uwezo wa mtu. Si Sunna ya kufanya mara moja moja. Hivyo, kama unataka kuingia katika watu wanaohesibaiwa Mutahajjiduun au Wanao Simama usiku kumuabudu Allah na kufanya ibada, basi bora ama uswali rakaa chache unazoweza kudumisha kila siku usiku, au ibada yoyote ile ambayo utaweza kuidumisha, kadiri ya uwezo wako. Hata kama utalala, kisha uamke na kuswali RAKAA MOJA TU YA WITRI, basi wewe ni Mutahajjid na Umesimama Usiku kwa Ibada.
No comments:
Post a Comment